Friday, 18 September 2015

Amenipanda Lyrics by Jemimah Thiong’o

Amenipanda Lyrics by Jemimah Thiong’o

Chorus:
Bwana asema, amenipanda mimi
Kando ya mito yenye maji mengi
Bwana asema, amenipanda mimi
Kando ya mito yenye maji mengi

Verse 1:
Ni Bwana alonipanda, kwa mikono yake Baba
Kando ya mito yenye rehema na baraka
Kunipalilia Baba, sikosi mbolea maji
Naishi nikiamini, siwezi nyauka nimepandwa ee

(Chorus)

Verse 2:
Kweli Baba wa rehema, amenipanda mimi
Baraka zanifuata kokote niendako
Amenipa uhai, akalinda afya yangu
Ndiposa nashuhudia, sifa alozipanda Mungu wangu

(Chorus)

Verse 3:
Imani ya wokovu, Hushinda majaribu
Hiyo ni baadhi ya mito nilopandwa kwayo
Mambo yangu yote baba, hupanga kwa utaratibu
Kwa maana anijali, aliyenipanda Mungu wangu wee

(Chorus)

Verse 4:
Hakuna juu mbinguni, wala chini duniani
Anayeshinda Mungu muumba mpanzi wangu
Hunizunguka mimi, kwa damu ya mwanao
Hunilinda vyema, sipati madhara kwani nimepandwa ee

(chorus)

No comments:

Post a Comment